Jukwaa La Michezo

  • Autor: Vários
  • Narrador: Vários
  • Editora: Podcast
  • Duração: 9:33:43
  • Mais informações

Informações:

Sinopse

Makala haya yanaangazia maendeleo ya michezo mbalimbali Ulimwenguni na pia huwa haiwaweki kando wanamichezo waliobobea na vilevile kufanya uchanganuzi wa kina wa michezo wakati wa mashindano mbalimbali. 

Episódios

  • AFCON 2025: Uganda, Tanzania kundi moja katika mashindano ya mwezi Disemba

    01/02/2025 Duração: 23min

    Hii leo tumeangazia yaliyozungumziwa kwenye mkutano mkuu wa jinsia wa Afrika Mashariki jijini Nairobi, shirikisho la kimataifa la mchezo wa baiskeli yapinga madai kuwa Rwanda itapokonywa haki za kuandaa mashindano ya chipukizi ya dunia mwezi Septemba kufuatia mzozo unaoendelea DRC, uchambuzi wa droo ya AFCON 2025, maandalizi ya CHAN 2024 tarehe mpya zatajwa na uchaguzi wa CAF mwaka huu. Pia tumechabua hatua ya mchujo mechi za Ligi ya Mabingwa Ulaya na tetesi za uhamisho ulaya.

  • Ligi kuu ya Tanzania bara imetajwa nafasi ya nne barani Afrika na 57 duniani

    25/01/2025 Duração: 23min

    Jioni hii kwenye makala ya Jukwaa la Michezo tumeangazia Congo kufutiliwa kushiriki mashindano ya CHAN 2024, kufutwa kazi kwa kocha wa Rwanda Torsten Spittler, uwanja mpya wa Talanta jijini Nairobi unaendelea kupiga hatua kwenye ujenzi huku ligi ya Tanzania ikitajwa nafasi ya nne katika orodha ya ligi bora Afrika, Kenya yang'ara mashindano ya chipukizi ya tenisi, msururu wa raga ya dunia mkondo wa tatu, fainali za Australian Open na tetesi za uhamisho ulaya na Afrika.

  • Droo ya CHAN 2024: Kenya yapangwa kundi gumu zaidi, mashindano ya Agosti 2025

    18/01/2025 Duração: 23min

    Kipindi cha leo kimeangazia pakubwa droo ya mashindano ya CHAN 2024; adhari ya kuahirishwa kwa kipute na uchambuzi wa makundi. Pia tumetupia jicho raundi ya sita hatua ya makundi mechi za klabu bingwa Afrika, fainali ya mashindano mapya ya wasichana U17, Shujaa yataja kikosi chake cha mkondo wa Perth 7s, Kipchoge akilenga taji la tano la London Marathon, Tyson Fury astaafu ndondi kwa mara ya pili pamoja na mashindano ya tenisi ya Australian Open yakiingia hatua ya robo fainali. Kulingana na droo iliyofanyika Jumatano usiku katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Kenyatta (KICC) jijini Nairobi nchini Kenya, Harambee Stars imepangwa katika 'kundi la kifo' ambapo itamenyana na mabingwa mara mbili Morocco (2018 na 2020) na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (2009 na 2016)."Tuko kwenye kundi la kifo," Mariga alikiri, akibainisha uimara wa wapinzani wao."Hizo ni timu kubwa na inamaanisha lazima tuweke juhudi zaidi katika maandalizi."“Wapinzani wetu ni wagumu, tutashiriki mashindano haya kwa mara ya kwanza lakini ha

  • CHAN 2024: Uwanja wa Nyayo nchini Kenya waidhinishwa na CAF kuandaa mashindano

    11/01/2025 Duração: 23min

    Tuliyokuandalia jioni hii ni pamoja na uchambuzi wa mashindano ya Mapinduzi, tetesi za uhamisho Afrika Mashariki, raundi ya tano ya mechi za klabu bingwa Afrika, maandalizi ya CHAN 2024, uhamisho wa wachezaji ulaya na mashindano ya tenisi ya Australian Open.

página 2 de 2